Rapa wawili maarufu wa Nigeria wakamatwa na dawa za kulevya

Rapa hao wawili walisainiwa mwaka jana kwenye lebo ya muziki ya rappa maarufu wa Nigeria na nyota wa Afropop Naira Marley.

0
Msanii Mohbad

Wakala wa mihadarati nchini Nigeria siku ya Alhamisi waliwakamata waimbaji wawili maarufu na wengine wanne wakiwa na dawa haramu katika uvamizi wa alfajiri katika nyumba yao katika kitovu cha kibiashara cha Lagos, afisa mmoja alisema.

Msemaji wa Shirika la Kitaifa la Kupambana na Dawa za Kulevya (NDLEA) Femi Babafemi aliiambia AFP bangi na aina ya dawa ya kulevya iitwayo ‘Molly’ zilipatikana na wasanii wa rapa Zinoleesky na Mohbad na washukiwa wengine wanne katika makazi yao na kwenye gari.

‘Maafisa wetu walivamia nyumba katika mtaa wa Idado asubuhi ya leo,’ alisema.

“Washukiwa sita — wanaume wanne na wanawake wawili — walichukuliwa. Kiasi cha bangi na Molly zilipatikana kutoka kwa nyumba na gari lao.”

Mohbad na Zinoleesky ni rapa wawili maarufu na nyimbo zao ni maarufu nchini, na muziki wao unasikizwa katika bara zima na ulimwenguni kote.

Wimbo maarufu wa Mohbad ‘Feel Good’ umetazamwa zaidi ya milioni nne kwenye Youtube.

Rapa hao wawili walisainiwa mwaka jana kwenye lebo ya muziki ya rappa maarufu wa Nigeria na nyota wa Afropop Naira Marley.

Marley, ambaye pia alihusika na tuhuma za ulaghai mtandaoni, alielezea ghadhabu yake kutokana na kukamatwa kwa wawili hao kwenye taarifa yake Instagram.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted