Finland imetajwa kama nchi yenye furaha zaidi duniani kwa mwaka wa tano

Finland inajulikana kwa huduma zake za umma zinazofanya kazi vizuri, imani iliyoko katika mamlaka na viwango vya chini vya uhalifu na usawa kati ya jamii.

0
 
Finland imetajwa kuwa nchi yenye furaha zaidi duniani kwa mwaka wa tano mfululizo, katika ripoti ya kila mwaka inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa ambayo tena iliiweka Afghanistan kama nchi isiyo na furaha, ikifuatiwa kwa karibu na Lebanon.

Serbia, Bulgaria na Romania zilirekodi ongezeko kubwa zaidi katika ustawi wa raia wake.
Nchi ambazo zilishuka katika viwango vya furaha katika jedwali la Furaha ya Dunia, iliyotolewa Ijumaa, ilikuja Lebanon, Venezuela na Afghanistan.

Lebanon, ambayo inakabiliwa na mdororo wa kiuchumi, ilishuka hadi ya pili kutoka mwisho katika orodha ya mataifa 146, chini kidogo ya Zimbabwe.

Afghanistan iliyokumbwa na vita, ambayo tayari inashikilia nafasi ya chini katika jedwali imeshuhudia mzozo wake wa kibinadamu ukiongezeka tangu Taliban kuchukua madaraka tena Agosti iliyopita.

Shirika la Umoja wa Mataifa la UNICEF linakadiria kuwa watoto milioni moja walio chini ya miaka mitano wanaweza kufa kwa njaa msimu huu wa baridi ikiwa hawatasaidiwa.
“Hii (faharisi) inatoa ukumbusho wa kina wa athari za vita kwa watu wengi,” mwandishi Jan-Emmanuel De Neve alisema.

Ripoti ya Dunia ya Furaha, sasa katika mwaka wake wa 10, inategemea tathmini ya watu wenyewe ya furaha yao, pamoja na data za kiuchumi na kijamii.
Inapeana alama ya furaha kwa kipimo cha sifuri hadi 10, kulingana na wastani wa data katika kipindi cha miaka mitatu.

Toleo hili la hivi punde lilikamilishwa kabla ya uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.
Wazungu wa Ulaya Kaskazini kwa mara nyingine tena walitawala nafasi za juu — huku Danes wakiwa nafasi ya pili nyuma ya Wafini, wakifuatiwa na Waaislandi, Waswizi na Waholanzi.

Marekani ilipanda kwa nafasi tatu hadi ya 16,nafasi moja mbele ya Uingereza, huku Ufaransa ikipanda hadi nafasi ya 20, nafasi yake ya juu zaidi.

Pamoja na hali ya kibinafsi ya ustawi wa mtu, kulingana na kura za Gallup katika kila nchi, alama ya furaha huzingatia Pato la Taifa, usaidizi wa kijamii, uhuru wa kibinafsi na viwango vya rushwa.
Mwaka huu waandishi pia walitumia data kutoka kwa mitandao ya kijamii kulinganisha hisia za watu kabla na baada ya janga la UVIKO-19.

Walipata “ongezeko kubwa la wasiwasi na huzuni” katika nchi 18 lnakushuka kwa hisia za hasira.
Somo la Ripoti ya Dunia ya Furaha kwa miaka mingi ni kwamba usaidizi wa kijamii, ukarimu kwa mtu na mwenzake na uaminifu serikalini ni muhimu kwa ustawi,” ripoti ya mwandishi Jeffrey Sachs aliandika, “Viongozi wa dunia wanapaswa kuzingatia.”

Ripoti hiyo iliibua hisia fulani ilipoiweka Ufini kwa mara ya kwanza katika orodha yake ya kwanza mwaka wa 2018. Watu wengi kati ya milioni 5.5 wa nchi hiyo ya Nordic wanajieleza kuwa watu wasio na utulivu na wanaokabiliwa na hali ya huzuni.

Nchi hiyo inajulikana kwa huduma zake za umma zinazofanya kazi vizuri, imani iliyoenea katika mamlaka na viwango vya chini vya uhalifu na usawa kati ya jamii.
In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted