Tarehe muhimu katika miaka 70 ya uongozi wa Malkia Elizabeth II

Mnamo Februari 6, Malkia Elizabeth II anakuwa kiongozi wa kwanza katika historia ya Uingereza kutawala kwa miaka 70.

0
Malkia Elizabeth II wa Uingereza asimama kwenye Balcony ya Buckingham Palace wakati wanajeshi wakipita wakati wa Gwaride la kusheherekea Kuzaliwa kwa Malkia, Trooping the Colour, kama sehemu ya sherehe za jubilee ya platinamu ya Malkia Elizabeth II, huko London mnamo Juni 2. (Photo by Jonathan Brady / POOL / AFP)

Malkia Elizabeth II ndiye kiongozi ambaye ameongoza kwa muda mrefu zaidi katika historia ya Uingereza na mwaka huu anasherehekea mwaka wake wa 70 uongozini.

1926: Kuzaliwa kwake

Elizabeth Alexandra Mary Windsor alizaliwa saa 2:40 asubuhi mnamo Aprili 21, 1926 huko Mayfair, katikati mwa London.

Yeye ndiye mtoto wa kwanza wa Duke na Duchess wa York, ambaye atakuwa Mfalme George VI na Malkia Elizabeth, Mama wa Malkia.

1940: Kuhamia Windsor

Ujerumani ya Nazi ilipopiga kwa mabomu mji mkuu wa Uingereza, Elizabeth na dadake mdogo, Princess Margaret, walihamia Windsor Castle, magharibi mwa London, kwa usalama wao.

Wakati wa Vita vya Kidunia vya pili, alijifunza kuwa fundi wa magari ya jeshi.

1947: Ndoa na familia

Princess Elizabeth aliolewa na Prince Philip huko Westminster Abbey

Mtoto wao wa kwanza, Prince Charles, alizaliwa mwaka wa 1948. Binti, Anne, alizaliwa mwaka wa 1950, akifuatiwa na Andrew mwaka wa 1960 na Edward mwaka wa 1964.

1952: Mwanamfalme hadi Malkia

Princess Elizabeth, mwenye umri wa miaka 25, atembelea Kenya na Philip, babake anapokufa akiwa na umri wa miaka 56 mnamo Februari 6, 1952. Anakatisha safari hiyo na kukimbilia Uingereza.

1953: Kutawazwa

Anatawazwa kuwa Malkia katika Westminster Abbey mnamo Juni 2, 1953, mbele ya wageni 8,500.

Sherehe hiyo inatazamwa kote duniani

1977: Silver Jubilee

Malkia anathibitisha tena kiapo cha huduma ya maisha kwa Uingereza na Jumuiya ya Madola kwenye hotuba aliyotoa awali alipokuwa na umri wa miaka 21 mnamo 1947.

Anazuru nchi na Jumuiya ya Madola.

1992: ‘Annus horribilis’

Prince Charles anajitenga na Princess Diana, na Andrew anaachana na mkewe, Sarah.

Binti pekee wa malkia, Princess Anne, anataliki mumewe, Mark Phillips.

Windsor Castle pia inaharibiwa vibaya na moto.

Malkia anaita miezi hiyo 12 yake “muda mbaya sana”

1997: Kifo cha Diana

Kifo cha Diana katika ajali ya gari mnamo Agosti 31, 1997 kilitikisa familia ya kifalme, na kusababisha ukosoaji wa malkia aliyendelea kukaa Balmoral huko Scotland baada ya kifo hicho.

Hatimaye anarudi Buckingham, ambako bendera ya Uingereza Union Jack inashushwa hadi nusu mlingoti, na anatoa rambirambi zake kwa Diana kupitia televisheni, na kusaidia kutuliza hasira ya umma.

2002: Golden Jubilee

Sherehe za miaka 50 ya uongozi wa malkia unakuja katika mwaka uleule wa vifo vya mama yake na dadake mdogo Margaret, na kuonyesha uungaji mkono wa umma kwa ufalme.

Umati mkubwa wa watu wakusanyika kwenye The Mall katikati mwa London kumtazama mpiga gitaa wa Malkia Brian May akicheza wimbo wa taifa kutoka kwenye paa la Buckingham Palace kabla ya tamasha la pop lililojaa nyota wa sanaa.

2011: Ziara ya jimbo la Ireland

 Ziara ya hadhi ya juu ya malkia nchini Ireland ni ya kwanza kufanywa na kiongozi wa Uingereza tangu Jamhuri ya Ireland ijinyakulie uhuru wake mwaka wa 1922.

Hotuba ya Kiayalandi, pamoja na ishara nyinginezo, yasaidia kuhimiza maridhiano na kuimarisha mchakato wa amani huko Ireland Kaskazini, baada ya miaka mingi ya mzozo kuhusu utawala wa Uingereza.

 2012: Olimpiki na Diamond Jubilee

Malkia na washiriki wengine wakuu wa familia ya kifalme wanatembelea kila eneo la Uingereza kuadhimisha miaka 60  uongozini.

Taa zawashwa kote nchini na shindano la mtoni lafanyika London.

Jambo la kushangaza kwa watu baada ya Malkia kushiriki kwenye kipindi kifupi na mwigizaji wa James Bond Daniel Craig katika sherehe za ufunguzi wa michezo ya Olimpiki ya 2012 London.

2021: Covid, Philip, hofu ya kiafya

Janga la coronavirus linamlazimisha malkia anayezeeka kujitenga huko Windsor, ambapo anajitokeza hadharani tu kupitia video.

Prince Philip alikufa akiwa na umri wa miaka 99 mnamo Aprili 2021, baadaye mwaka huo hofu inakua kuhusu afya ya malkia baada ya kulazwa hospitalini na kulazimika kupunguza majukumu yake.

2022: Platinum Jubilee

Mnamo Februari 6, anakuwa kiongozi wa kwanza katika historia ya Uingereza kutawala kwa miaka 70.

Siku nne za sherehe zapangwa mapema Juni.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted