Mgombea wa Upinzani Nigeria amteua mgombea mwenza katika uchaguzi wa 2023

Abubakar, mgombea wa chama cha Peoples Democratic Party (PDP) anawania kiti cha urais kwa mara ya sita na atakuwa anakabiliana na mgombea wa chama tawala na gavana wa...

0
Atiku Abubakar mgombea urais wa chama cha PDP katika uchaguzi wa 2023 Nigeria. (Photo by PIUS UTOMI EKPEI / AFP)

Mgombea wa upinzani nchini Nigeria Atiku Abubakar siku ya Alhamisi alimteua gavana wa jimbo linalozalisha mafuta la Delta kuwa mgombea mwenza wake katika uchaguzi wa 2023.

Abubakar, mgombea wa chama cha Peoples Democratic Party (PDP) anawania kiti cha urais kwa mara ya sita na atakuwa anakabiliana na mgombea wa chama tawala na gavana wa zamani wa Lagos Bola Tinubu katika uchaguzi wa Februari.

Nigeria inakabiliwa na changamoto kubwa za kiusalama na kiuchumi miezi minane kabla kufanyika kwa uchaguzi wa kumpata rais atakayechukua nafasi ya Rais Muhammadu Buhari anayestaafu baada ya mihula miwili.

Abubakar, 75, Muislamu kutoka kaskazini mashariki mwa Jimbo la Adamawa, alisema amemtaja gavana wa Delta Ifeanyi Okowa kama makamu wake wa rais na mgombea mwenza.

“Niliweka wazi kwamba mgombea mwenza wangu angekuwa na uwezo wa kunirithi iwapo lolote litakapotokea, yaani, rais anayenisubiri,” Abubakar aliuambia mkutano wa waandishi wa habari mjini Abuja.

Mgombea wa chama tawala cha All Progressives Congress au APC Bola Tinubu ni Muislamu wa kusini, bado hajatangaza chaguo lake, lakini anatarajiwa kuchagua mgombea mwenza kutoka mikoa ya kaskazini.

Swali kuu katika maandalizi ya mchujo wa chama mwezi uliopita na mwezi huu lilikuwa kugawa maeneo mpango ambao haukuandikwa unaotaka uongozi wa urais unabadilika kati ya kusini na kaskazini.

Baada ya mihula miwili na Buhari ambaye ni muislamu kutoka kaskazini, wengi wanatarajia kushinda wa rais wa kusini.

PDP ilivunja mila ya kuchagua mgomvea kutoka kusini na kumtaja mgombea wa kaskazini.

Makubaliano hayo — na tabia ya wagombea kuchagua wenza kutoka dini na maeneo tofauti na wao — inaonekana kama njia ya kuleta usawa katika nchi iliyogawanyika kati ya kusini yenye Wakristo wengi na kaskazini yenye Waislamu wengi.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted