Augustine Lyatonga Mrema Mwanasiasa aliyetamba kwenye ulingo wa siasa na kuacha gumzo kila mahali 

Mrema ambaye hivi sasa hayupo katika uso wa dunia kufuati kifo chake kilichotokea Agosti 21,2022 katika hospitali ya Taifa Muhimbili nchini Tanzania alipokuwa amelazwa akipokea matibabu atakumbukwa kwa mengi hasa katika nguvu yake ya kujenga hoja za kisiasa dhidi ya watawala wa nchi.