#KENYA: Mahakama kuu yasitisha uamuzi wa kuvishutumu vituo sita vya televisheni kwa kuripoti maandamano ya upinzani

Katiba inasema kanuni za programu zinahitaji kuangaliwa mara moja kila baada ya miaka miwili lakini mamlaka hiyo ilizipitia kwa mara ya mwisho mwaka 2019 ambao ni zaidi ya...

0
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Kenya (CA) Ezra Chiloba

Mahakama Kuu imesitisha uamuzi wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini Kenya wa kuvishutumu vituo sita vya televisheni kwa kuripoti maandamano ya Azimio ya Jumatatu.

Hii ni baada ya baraza la watetezi kuhamia kortini kutaka kuzuwia Mamlaka ya Mawasiliano kutekeleza uamuzi wake wa kushutumu vituo sita vya televisheni kwa kuangazia maonyesho ya Azimio Jumatatu.

Jaji J Chigiti ametoa ruhusa kwa Taasisi ya Katiba kuwasilisha mapitio ya mahakama ili kusitisha lawama dhidi ya vituo vya televisheni.

Kesi hiyo itatajwa Mei 10 kwa maelekezo zaidi.

Kupitia kwa wakili Dudley Ochiel, Taasisi ya Katiba inahoji kuwa Mamlaka ya Mawasiliano imevishutumu vituo hivyo kinyume na katiba na kinyume cha sheria.

Ochiel anasema kuwa uamuzi wa mamlaka hiyo unakiuka sheria za haki asilia na kuongeza kuwa hakuna hata chombo kimoja cha habari kati ya hivyo sita kilichosikizwa kuhusu uamuzi wa kuwashutumu.

Katiba inasema kanuni za programu zinahitaji kuangaliwa mara moja kila baada ya miaka miwili lakini mamlaka hiyo ilizipitia kwa mara ya mwisho mwaka 2019 ambao ni zaidi ya miezi 18 iliyopita.

“Mbali na hilo, bila kuchapishwa kwenye gazeti la serikali, kanuni za programu sio sheria. Mbaya zaidi, msimbo wa programu uliisha muda wake Septemba 2021 bila kuanza kutumika,” zinasomeka nyaraka za mahakama.

Ochiel anahoji kuwa suala hilo ni la dharura kwa sababu mamlaka hiyo imetishia kuwajibika chini ya vipengee husika vya sheria ikiwa ni pamoja na kubatilishwa.

Katika taarifa yake Jumatano, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Ezra Chiloba alisema matangazo hayo yanaonyesha matukio ambayo yanaweza kusababisha hofu au uchochezi kwa umma, na kutishia amani na mshikamano nchini.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted