Shahidi Akwamisha Kesi ya Lissu, Mahakama Yaahirisha hadi Jumatatu
Lissu ameendelea kupinga kuahirishwa kwa kesi hiyo akidai kuwa upande wa Jamhuri umekuwa ukiomba kuahirishwa kwa kesi mara kwa mara bila Mahakama kuchukua hatua dhidi yao.
Lissu ameendelea kupinga kuahirishwa kwa kesi hiyo akidai kuwa upande wa Jamhuri umekuwa ukiomba kuahirishwa kwa kesi mara kwa mara bila Mahakama kuchukua hatua dhidi yao.
Shahidi wa kificho katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, ameieleza Mahakama Kuu kuwa ana hofu ya kutoa ushahidi wake hadharani, akisema suala hilo ni “very sensitive” na kwamba wafuasi wa chama hicho wanaweza kuwa na hasira naye licha ya kuwa na mahusiano mazuri na Viongozi wakuu wa Chadema.
Lissu: Shahidi, nataka kwanza nianze na maswali yangu ya jana kuhusu tofauti kati ya ushahidi ulioutoa kwenye maelezo ya polisi na ushahidi ulioutoa kizimbani. Waeleze Waheshimiwa Majaji kama unaamini maelezo yako yanapaswa kuaminiwa na mahakama.
Shahidi: Ni kweli.
Lissu: Waeleze Waheshimiwa Majaji kama kuna mahali umeeleza sababu za tofauti kati ya ulichoandika na ulichosema mahakamani.
Shahidi: Hakuna mahali.
Shahidi alikiri kuwa jina la Tundu Lissu lilikuwepo katika maelezo hayo, lakini alikanusha kuwa aliandika kwamba aliona jalada lililomtaja Tundu Antipus Lissu alipofika kwa Naibu ZCO George Bagemu.
Shahidi wa nne katika kesi ya Kikatiba ambaye ni Mkuu wa Gereza la Ukonga Edward Shabani amesema hafahamu wala hajui kwamba Tundu Lissu ni Wakili kitaaluma na aliwahi pia kuwa Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika(TLS).