Africa Crime & Justice East Africa People Politics Tanzania

Shahidi wa Kificho Asema Ana Hofu Kutoa Ushahidi Hadharani Katika Kesi ya Uhaini ya Lissu

Shahidi wa kificho katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, ameieleza Mahakama Kuu kuwa ana hofu ya kutoa ushahidi wake hadharani, akisema suala hilo ni “very sensitive” na kwamba wafuasi wa chama hicho wanaweza kuwa na hasira naye licha ya kuwa na mahusiano mazuri na Viongozi wakuu wa Chadema.

Africa Crime & Justice East Africa Tanzania

Kesi ya Lissu: Shahidi Akiri Kutoeleza Tofauti ya Ushahidi wa Maelezo ya Polisi na Aliotoa Mahakamani

Lissu: Shahidi, nataka kwanza nianze na maswali yangu ya jana kuhusu tofauti kati ya ushahidi ulioutoa kwenye maelezo ya polisi na ushahidi ulioutoa kizimbani. Waeleze Waheshimiwa Majaji kama unaamini maelezo yako yanapaswa kuaminiwa na mahakama.
Shahidi: Ni kweli.
Lissu: Waeleze Waheshimiwa Majaji kama kuna mahali umeeleza sababu za tofauti kati ya ulichoandika na ulichosema mahakamani.
Shahidi: Hakuna mahali.