Africa East Africa

UN yaipongeza Kenya kwa kushiriki Uchaguzi Mkuu kwa amani

Taarifa iliyotolewa na msemaji wa Katibu Mkuu Stéphane Dujarric kutoka New York nchini Marekani imesema, Katibu Mkuu anatambua kazi muhimu iliyofanywa na mamlaka ya Kenya pamoja na mashirika mengi yote yanayohusika na usimamizi wa uchaguzi, ushirikishwaji wa wadau mbalimbali wa kitaifa na dhamira ya dhati isiyoyumbishwa ya wapiga kura kutekeleza haki yao ya kikatiba ya kupiga kura.