Kiongozi wa upinzani Uganda Kizza Besigye alazwa ICU baada ya kuanguka mahakamani
Besigye mwenye umri wa miaka 70, anayekabiliwa na mashtaka ya uhaini kwa madai ya kupanga njama dhidi ya Rais Yoweri Museveni, alianguka Jumatano wakati wa kusikilizwa kwa kesi yake baada ya kukataa mawakili aliopangiwa na serikali. Kabla ya kuanguka, alikuwa akilalamikia kuzuiwa kwa mawakili wake binafsi kumwakilisha.