Chadema yawateua watiania 73 kuwania viti mbali mbali kanda ya Pwani

Watia nia 73 wameteuliwa na Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwania nafasi mbalimbali katika kanda tatu za chama hicho.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya usaili wa watia nia 79 kutoka Kanda ya Pwani inayoundwa na mikoa ya (Dar es Salaam na Pwani), Kusini (Mtwara, Ruvuma na Lindi) na ya Pemba (Kaskazini Pemba na Kusini Pemba) uliofanyika  Septemba 17, 2024

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema amesema leo Septemba 18 kuwa, kati ya watia nia 79 ni 73 walioteuliwa

Mrema amesema Kamati Kuu ikiongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe imefanya uteuzi huo kwa mujibu wa Katiba ya Chadema na Kuteua wagombea wa Uenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Mtunza Hazina wa Kanda

Amesema katika kanda zote walioomba nafasi ya uenyekiti na makamu wote wamepenya, akieleza sita walioenguliwa kuendelea na mchakato huo hawakukidhi vigezo kulingana na nafasi walizoomba

Waliopitishwa Kanda ya Pwani ni uenyekiti, Boniface Jacob na Gervas Lyenda, huku makamu mwenyekiti ni Shekh Ally Mohamed ‘Kadogoo’ na Baraka Musa