Rais wa Marekani Donald Trump amesema Marekani “itachukua udhibiti” na kuumiliki Ukanda wa Gaza.
![](https://mwanzotv.com/wp-content/uploads/2025/02/AFP__20250205__36X37W8__v1__HighRes__UsIsraelDiplomacyNetanyahuTrump-scaled.jpg)
Trump aliyasema haya wakati alipokuwa mwenyeji wa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu Jumanne kwa ajili ya mazungumzo muhimu ya usitishaji mapigano na wanamgambo wa Hamas.
Endapo hilo la Marekani kuimiliki Gaza litafanyika,basi hatua hiyo itakuwa imeivunja sera ya miongo kadhaa ya Marekani kwa mzozo wa Israel na Palestina.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mkutano huo na Netanyahu, Trump vile vile alirudia kauli yake kwamba Wapalestina wanastahili kuondoka Gaza iliyoharibiwa vibaya kwa vita na wakaanze maisha mapya ya kudumu katika mataifa mengine ya Mashariki ya Kati kama Misri na Jordan, licha ya Wapalestina na mataifa hayo mawili yote kulikataa pendekezo hilo.
Up
Rais huyo wa Marekani alisema Marekani itaisafisha Gaza kwa kuyaondoa mabomu ambayo hayajalipuka na kuleta ustawi wa kiuchumi ambao utabuni ajira na makao chungunzima kwa watu watakaoishi katika eneo hilo.
Trump vile vile aliongeza kwamba haondoi uwezekano wa kupeleka jeshi la Marekani kusaidia katika ujenzi mpya wa Gaza.