Jaribio la Mauaji ya Trump: Kilichotokea

Donald Trump alinusurika kwa tundu la sindano katika jaribio la mauaji kwenye mkutano wa kisiasa Jumamosi. Shirika la upelelezi ya nchini Marekani (FBI) sasa inachunguza tukio hilo.

Kilivyotokea:

  • Trump, akiwa amevaa shati jeupe, koti jeusi, na kofia nyekundu ya MAGA, alikuwa akizungumza dhidi ya uhamiaji haramu wakati risasi zilipoanza kurindima saa 12:08 jioni.
  • Trump alishika sikio lake la kulia huku risasi nne zikifyatuliwa, ikifuatiwa na risasi ya tano na ya sita.
  • Maajenti wa Secret Service walimzunguka Trump haraka huku akiinama nyuma ya mimbari.
  • Risasi zaidi zilifyatuliwa, zikisababisha hofu kwa umati.
  • Ndani ya sekunde 22, vikosi vya usalama vilipanda jukwaani na Trump aliinuliwa na maajenti.
  • Trump aliwahakikishia umati yuko salama, akaongozwa kutoka jukwaani, akasindikizwa hadi kwenye gari la usalama.

Jibu la Trump:

  • Trump alichapisha kwenye Truth Social saa 2:42 usiku, akisema alipigwa risasi na kuhisi risasi ikipenya sikio lake la kulia.
  • Rais Joe Biden alifahamishwa na kulaani tukio hilo, akikatisha mapumziko yake ya ufukweni kurudi Washington.

Mshambuliaji Alitambulika:

  • FBI ilimtambulisha mshambuliaji kama Thomas Matthew Crooks, kijana wa miaka 20 kutoka Bethel Park, Pennsylvania.
  • Crooks, aliyesajiliwa kama Republican, aliwahi kuchangia dola 15 kwa kundi la wapiga kura wa mrengo wa kushoto.
  • Mshambuliaji alipiga risasi kutoka juu na alidhibitiwa na maajenti.

Waathiriwa:

  • Mshambuliaji na mshiriki mmoja waliuawa; watazamaji wawili walijeruhiwa vibaya.
  • Mashuhuda waliripoti kumuona mtu aliyepigwa risasi kichwani na mwanamke mwingine aliyepigwa risasi mkononi.

Polisi wa eneo hilo walijibu ripoti za shughuli za kutiliwa shaka lakini hawajatoa maelezo zaidi.