Shahidi augua ghafla akiwa kizimbani wakati akitoa ushahidi
Ni shahidi wa 10 katika kesi ya ugaidi inayomkabili mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na wenzake watatu.
Ni shahidi wa 10 katika kesi ya ugaidi inayomkabili mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na wenzake watatu.
Ni katika kesi ya Ugaidi inayomkabili mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe na wenzanke watatu
Shahidi wa kwanza upande wa utetezi Adam Kasekwa (Mshitakiwa wa 2), amepata kigugumizi cha kujibu maswali aliyokuwa akiulizwa na Wakili wa Serikali Abdallah Chavula. Hayo yamejiri leo katika Kesi Na.16/2021 inayowakabili Freeman Mbowe na wenzake 3, ambapo shahidi huyo ametoa ushahidi wake mbele Jaji Mustapha Siyani katika Mahakama Kuu Division ya Uhujumu Uchumi na Rushwa Ni baada ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Adballah Chavula, alipomuuliza mshtakiwa huyo mahakama ichukue kauli ipi kati ya maelezo yake aliyowahi kutoa mahakamani hapo, akidai alitoa maelezo yake ya onyo katika Kituo cha Polisi Mbweni mkoani Dar es Salaam, kwa mateso na maelezo aliyotoa akidai, alichukuliwa maelezo yake baada ya kutishwa na sio kuteswa.