Wamaasai Tanzania wasilisha kesi mahakamani kuhusu eneo la ulinzi la wanyamapori

Wafugaji wa Kimaasai wamewasilisha kesi mahakamani dhidi ya serikali ya Tanzania, kupinga uamuzi wake wa kuzingira ardhi kwa ajili ya ulinzi wa wanyamapori, wakili anayewakilisha jamii hiyo alisema Jumatano.

Jamii ya wahamaji wa Loliondo Wilaya ya Kaskazini ya Ngorongoro wameishutumu serikali kwa kujaribu kuwalazimisha kuondoka kwenye ardhi ya mababu zao ili kuandaa safari na uwindaji.

Lakini serikali imekataa shutuma hizo, ikidai inataka “kulinda” kilomita za mraba 1,500 (maili za mraba 580) za eneo hilo kutokana na shughuli za kibinadamu.

“Kesi hiyo ni muhimu kwa wakazi wa Loliondo,” wakili Yonas Masiaya aliambia AFP katika ujumbe wake.

“Eneo hilo ni marufuku kabisa kufuga wala kuingia na wakazi wa eneo hilo walikuwa wakilitegemea kwa malisho, maji, matambiko na mitishamba,” alisema na kuongeza kuwa jamii inataka majaji kubatilisha uamuzi wa serikali.

Kesi hiyo iliwasilishwa mnamo Septemba,wiki chache kabla ya mahakama ya kikanda kutoa uamuzi kwa upande wa serikali katika ombi tofauti.Mahakama ya Afrika Mashariki yenye makao yake makuu jijini Arusha imeridhia uamuzi wa serikali katika hukumu iliyotangazwa Septemba 30 mwaka huu na kusema kuwa hakuna fidia iliyotokana na wafugaji hao kulalamika kufukuzwa katika ardhi yao.

Mvutano umeongezeka katika miezi ya hivi karibuni huku mapigano makali yakizuka mwezi Juni huko Loliondo kati ya polisi na waandamanaji wa Kimasai.

Zaidi ya waandamanaji kumi na wawili wa kimasai walishtakiwa kwa mauaji kutokana na kifo cha polisi katika makabiliano hayo.

Kihistoria, Tanzania imeruhusu jamii za kiasili kama vile Wamasai kuishi ndani ya baadhi ya hifadhi za taifa, ikiwemo eneo la hifadhi ya Ngorongoro, eneo la Urithi wa Dunia wa UNESCO.

Lakini mamlaka zinasema idadi yao inayoongezeka inavamia makazi ya wanyamapori na ilianza kuwahamisha wafugaji kutoka Ngorongoro mwezi Juni, na kuuita uhamishaji wa hiari.

Hatua hiyo imezua wasiwasi, huku timu ya wataalam huru walioteuliwa na Umoja wa Mataifa wakionya mwezi Juni kwamba “inaweza kuhatarisha maisha ya Wamasai kimwili na kiutamaduni.”

Tangu mwaka 1959, idadi ya watu wanaoishi Ngorongoro imeongezeka kutoka 8,000 hadi zaidi ya 100,000.

Kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa kusababisha ukame wa muda mrefu na mavuno machache ya mazao, shinikizo kwa wafugaji limeongezeka na kuwafanya waingie kwenye migogoro na wanyamapori kuhusu upatikanaji wa chakula na maji.

Mwaka 2009, maelfu ya familia za Wamasai zilihamishwa kutoka Loliondo ili kuruhusu kampuni ya safari ya Emirati, Otterlo Business Corporation, kuandaa safari za uwindaji huko.

Mwaka 2009, maelfu ya familia za Wamasai zilihamishwa kutoka Loliondo ili kuruhusu kampuni ya safari ya Emirati, Otterlo Business Corporation, kuandaa safari za uwindaji huko.