Polisi: Dogo Janja alifyatua risasi akijihami Arusha
Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha linaendelea na uchunguzi kuhusu tukio la kupigwa risasi kijana Bakari Halifa Daudi (18) katika eneo la Sombetini, jijini Arusha, linalomhusisha Mgombea Udiwani wa Kata ya Ngarenaro kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulaziz Abubakari Chande maarufu kama Dogo Janja.