Kenya yazindua mradi wa reli ya kisasa kutoka Naivasha hadi Malaba

Kenya inaanzisha upya upanuzi wa reli yenye thamani ya mabilioni ya Dola ambao ulifadhiliwa kupitia uwekaji wa mapato na hapo kufufua mradi ambao umekwama kwa zaidi ya miaka sita. Hii ilifuatia kukoma kwa mikopo ya awali kutoka China.

Rais wa Kenya William Ruto anasema reli hiyo itapunguza msongamano wa barabara kwa kuhamisha shehena kubwa kupitia usafari wa reli, na kupunguza gharama, kuokoa muda, na kuongeza usalama katika barabara kuu za nchi.

“Upanuzi wa Reli ya Kisasa Standard Gauge utaiweka Kenya kama kitovu cha biashara na vifaa vya kikanda, ikiunganisha Uganda, Rwanda, Burundi, Sudan Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Bandari ya Mombasa huku ikifungua uwezo wa kiuchumi wa Magharibi mwa Kenya,” Rais wa Kenya William Ruto alisema alipokutana na Mwenyekiti wa Kampuni ya Ujenzi ya Mawasiliano ya China, Song Hailiang katika Ikulu ya Nairobi.

“Pia itapunguza msongamano barabarani kwa kuhamisha shehena nyingi kutumia reli, kupunguza gharama, kuokoa muda, na kuboresha usalama katika barabara zetu kuu,” Rais Ruto aliongeza katika taarifa yake.

Lakini baada ya China kupunguza ufadhili wa miradi mikubwa ya miundombinu barani Afrika chini ya Mpango wake wa Ukanda na Barabara, mradi huo ulikwama karibu na mji wa Bonde la Ufa wa Naivasha, umbali wa zaidi ya kilomita 350 kufikia mpaka wa Uganda na kuchelewesha mpango wa kuunganisha mpaka na kuimarisha uhusiano wa kikanda na biashara.

Mwaka jana, Kenya na China zilijadiliana upya masharti ya mikopo iliyotumika kujenga awamu mbili za kwanza ili kupunguza ulipaji wa kila mwaka kwa Kenya.

Kenya ilibadilisha sheria yake kuruhusu matumizi ya kiasi kikubwa cha tozo ya maendeleo ya reli inayotozwa kwa mizigo inayobebwa kwenye njia iliyopo na inakadiriwa kuwa shilingi bilioni 35 (Dola milioni 270.27) kama pesa za mbegu kwa ajili ya ujenzi wa awamu mpya.

Bado kuna ushiriki wa China huku shirika la China Road and Bridge Corporation inayomilikiwa na serikali ikiwa mkandarasi, lilisema Shirika la Reli nchini Kenya.