Bashar al-Assad na familia yake wapewa hifadhi Urusi
Hayo yameelezwa Jumapili usiku na Ikulu ya Kremlin, iliyosisitiza kuwa makubaliano yamefikiwa ili kuhakikisha usalama wa kambi za kijeshi za Urusi nchini Syria. Awali Moscow ilisema kambi hizo ziko katika tahadhari kubwa lakini hakukuwa na kitisho dhidi yao kwa sasa.