Tanzania yatetea mpango wa uhamaji wa hiari Ngorongoro mbele ya UNESCO
Serikali ya Tanzania imeutetea mpango wa uhamaji wa hiari wa wakazi wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro mbele ya Kamati ya Urithi wa Dunia ya UNESCO, ikisema hatua hiyo inalenga kulinda haki za binadamu, kuhifadhi utu wa wananchi na wakati huo huo kuhakikisha uendelevu wa uhifadhi wa eneo hilo.