Bunge la Marekani laidhinisha muswada wa kutathmini upya uhusiano wake na Tanzania
Kamati ya Mahusiano ya Kigeni yabunge la Marekani imeidhinisha miswada mitano ya sera za mambo ya nje, ikiwemo muswada unaotaka kufanyika kwa tathmini ya kina ya uhusiano kati ya Marekani na Tanzania kufuatia kile wabunge wa Marekani wanachokitaja kuwa kuongezeka kwa vurugu za kisiasa na kudorora kwa demokrasia nchini humo.