Waandishi wa habari 272 walipata madhila katika kipindi cha miaka 10 nchini Tanzania
Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) Kajubi Mukajanga katika kongamano la miaka 30 ya siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yenye kauli mbiu ‘Uhuru wa Kujieleza kama Kichocheo cha Haki Nyingine za Binadamu’ kitaifa maadhimisho hayo yanafanyika visiwani Zanzibar.