Uganda yasitisha ushirikiano wa Kijeshi na Ujerumani kwa tuhuma za Uhaini
Jeshi la Uganda (UPDF) limetangaza kusitisha mara moja ushirikiano wa kijeshi na Ujerumani, likimtuhumu Balozi wa Ujerumani nchini humo, Matthias Schauer, kwa kuendesha “shughuli za kihaini” ndani ya taifa hilo la Afrika Mashariki.