Uchaguzi wa Nigeria 2023: Peter Obi ashinda Lagos dhidi ya Bola Tinubu katika matokeo ya awali

Mgombea urais wa chama cha tatu kwa ukubwa nchini Nigeria alisababisha ushindani mkali ambao ulizua ghadhabu kubwa kwa kushinda katika jiji kubwa zaidi la Lagos.

Peter Obi wa chama cha Labour amemshinda Bola Tinubu wa chama tawala katika eneo alilotoka, matokeo yaliyotangazwa na maafisa wa uchaguzi wa majimbo yanaonesha.

Hii ni mara ya kwanza tangu mwaka 1999 kwa chama hicho kinachoungwa mkono na Bw Tinubu, gavana wa Lagos mara mbili, kutoshinda jimbo hilo.

Lakini Bw Tinubu ameshinda majimbo matatu kati ya matano yaliyotangazwa kufikia sasa.

Zaidi ya watu milioni 87 walistahili kushiriki katika uchaguzi huo, na kulifanya zoezi kuwa kubwa zaidi katika taifa la kidemokrasia zaidi barani Afrika.

Chama tawala cha All Progressives Congress (APC) na PDP vimetawala Nigeria tangu kumalizika kwa utawala wa kijeshi mwaka 1999 lakini kwa sasa, Bw Obi kutoka chama kisichojulikana sana cha Labour anatarajiwa kuleta upinzani mkubwa katika mfumo wa vyama viwili.

Anaungwa mkono na vijana wengi, ambao ni theluthi moja ya wapiga kura waliojiandikisha.

Mgombea anahitaji kuwa na kura nyingi zaidi na robo ya kura zilizopigwa katika majimbo 25 kati ya 36 pamoja na Abuja ili kutangazwa mshindi.

Vinginevyo, kutakuwa na duru ya pili ndani ya siku 21 za kwanza katika historia ya Nigeria.