Africa East Africa

LHRC, TAS waitaka Klabu ya Simba kuomba radhi kwa udhalilishaji dhidi ya wenye ualbino.

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu(LHRC), kwa kushirikiana na Chama cha Watu wenye Ualbino Tanzania (TAS), kimelaani vikali kitendo kilichotokea Agosti 6, 2023 katika siku ya Simba Day, kinachohusisha matumizi ya mtu mwenye ualbino kwa mtindo unaofanana na mtu aliyevaa nepi iliyochafuka jukwaani mbele ya umati wa maelfu ya watu kwenye Uwanja wa Taifa akiwa nusu uchi.