Lissu ni ama afikishwe Mahakamani kesho ama aanze mgomo wa kula akiwa gerezani
Lissu ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema Taifa alikamatwa tarehe 9 Aprili 2025 majira ya saa za jioni akiwa Ruvuma muda mchache mara baada ya kumaliza mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Mbinga.Usiku huo huo alisafirishwa hadi Dar es Salaam chini ya ulinzi mkali wa maofisa wa polisi na kufikishwa katika kituo cha kati cha Polisi.