Chama tawala cha DRC kimemtaka Kabila aache kuingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo
Katika hotuba yake jana Jumapili, Katibu Mkuu wa chama cha Union for Democracy and Social Progress (UDPS), Augustin Kabuya, alimtuhumu Kabila kwa kuhusika na kundi la waasi la M23 linaloungwa mkono na Rwanda na kudai kuwa Kabila “aliletwa kwa nguvu kututawala” na kwamba hana mamlaka tena ya kutoa mafunzo kuhusu demokrasia.