Wakimbizi wa Congo wasimulia vifo na machafuko wakati vita vikianza upya
Maelfu wamekimbia huku raia wakijikuta tena katikati ya mapigano kati ya M23, jeshi la Congo na washirika wao.
Maelfu wamekimbia huku raia wakijikuta tena katikati ya mapigano kati ya M23, jeshi la Congo na washirika wao.
Katika hotuba yake jana Jumapili, Katibu Mkuu wa chama cha Union for Democracy and Social Progress (UDPS), Augustin Kabuya, alimtuhumu Kabila kwa kuhusika na kundi la waasi la M23 linaloungwa mkono na Rwanda na kudai kuwa Kabila “aliletwa kwa nguvu kututawala” na kwamba hana mamlaka tena ya kutoa mafunzo kuhusu demokrasia.
Kuchukuliwa kwa mji wa Walikale wenye wakazi takriban 60,000 mwishoni mwa siku ya Jumatano kunashiria kwamba kundi hili la wapiganaji limefika sehemu ya mbali kabisa magharibi kutoka eneo lao la awali tangu lilipojitokeza mwaka 2012.
Kikundi cha M23 kilichopatiwa msaada na Rwanda kimesema hakiwezi kushiriki katika mazungumzo ya amani na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) yaliyopangwa kufanyika leo Jumanne mjini Luanda, mji mkuu wa Angola, kufuatia vikwazo vya Umoja wa Ulaya dhidi ya baadhi ya viongozi wake wakuu.
Katika mahojiano alipoitembelea Kinshasa, Mwendesha Mashtaka Khan alikubali kushindwa kwa mfumo wa haki za kimataifa kuzuia ukatili wa kutisha ambao umekuwepo kwa miongo kadhaa katika eneo hili na kusema kuwa yeye ni “ana masikitiko makubwa kuhusu kuongezeka kwa ghasia.”
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) alisema Jumatatu kwamba zaidi ya watu 7,000 wamefariki mashariki mwa nchi hiyo tangu mwezi Januari, wakati kundi la M23 lililokuwa likiungwa mkono na Rwanda lilipochukua miji miwili mikubwa.
Rais wa Burundi alielekea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kwa mazungumzo na mwenyeji wake, Rais Felix Tshisekedi, kuhusu mgogoro unaoendelea mashariki mwa taifa hilo lenye eneo kubwa la Afrika ya Kati, vyanzo vingi vya habari vimesema.
Mapigano yalizuka tena leo Jumanne mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya mapumziko ya siku mbili, ambapo wapiganaji wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda walishambulia maeneo ya jeshi la Congo katika jimbo la South Kivu asubuhi, kwa mujibu wa vyanzo vya eneo na usalama vilivyosema.
Kundi la M23 linaloungwa mkono na Rwanda liliongeza mashambulizi yake siku ya Alhamisi kupitia mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na linaonekana kuwa na nia ya kuchukua mji muhimu, huku Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, akitoa wito wa amani.
Rais wa Angola alitoa wito Jumatano kwa “kuondolewa mara moja” kwa wanajeshi wa Rwanda kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na kwa viongozi wa nchi hizo mbili kukutana kwa dharura huko Luanda kujadili mgogoro huo.