ACT -Wazalendo:Polisi waachieni viongozi wa CHADEMA bila masharti
Chama cha ACT Wazalendo kimelaani na kukemea vikali vitisho vya Jeshi la Polisi na kukamatwa kwa viongozi wakuu wa CHADEMA na kuzuiwa kwa kongamano la vijana wa CHADEMA katika kuadhimisha siku ya vijana duniani iliyopangwa kufanyika leo Agosti 12, jijini Mbeya.