Hakimu Ndeyekobora aondolewa kusikiliza kesi ya Mfalme Zumaridi
Kuondolewa kwa hakimu huyo huenda kukawa ni majibu ya maombi yaliyowasilishwa Julai 28,2022 na mshtakiwa namba moja katika shauri hilo Mfalme Zumaridi kupitia kwa mawakili wake wakimtaka, Ndyekobora kujiondoa kusikiliza shauri hilo kwa kile walichodai mteja wao hana imani naye huku hakimu huyo akiweka ngumu kujiondoa kwa kile alichodai maombi hayo hayana mashiko.