East Africa Politics Tanzania

Dar kurejeshewa hadhi yake ya kuwa jiji

Februari 24, 2021, aliyekuwa Rais wakati huo Hayati John Magufuli alitangaza kulivunja jiji la Dar es salaam na kupandisha moja kati ya manispaa zake kuwa jiji. Raisi Magufuli alitangaza uamuzi huo wakati wa uzinduzi wa daraja la juu la Kijazi lililopo Ubungo,hafla iliyohudhuriwa na viongozi waandamizi kadhaa wa Serikali pamoja na wadau wengine wa maendeleo ya Tanzania.