Mpox yatangazwa kuwa ni dharura ya kiafya Afrika
Mlipuko huo umeenea katika nchi kadhaa za Kiafrika, haswa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambapo virusi vilivyoitwa Mpox au Homa ya Nyani viligunduliwa kwa mara ya kwanza kwa wanadamu mnamo 1970.
Mlipuko huo umeenea katika nchi kadhaa za Kiafrika, haswa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambapo virusi vilivyoitwa Mpox au Homa ya Nyani viligunduliwa kwa mara ya kwanza kwa wanadamu mnamo 1970.
Kwa mujibu wa Naibu Katibu Mkuu Bara kutoka chama cha Chadema bwana Benson Kigaila ni kwamba katika kundi kubwa la watu takribani 500 waliokamatwa na Polisi kati ya siku hizo mbili, wakiwemo viongozi wakuu wa chama hicho ni kwamba Makamu Mwenyekiti Bara, Tundu Lissu, Katibu Mkuu John Mnyika na Mwenyekiti Kanda ya Nyasa, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu wameumizwa vibaya kutokana na nguvu iliyotumika kuwakamata.
Katika taarifa ya Chadema iliyotolewa na John Mrema, Mkurugenzi wa Mawasiliano, Itikadi, Uenezi na Mambo ya Nje kupitia ukurasa wake wa X zamani Twitter, imeeleza viongozi hao walirudishwa kutoka jijini Mbeya walikokamatiwa na kurejeshwa Dar es salaam usiku chini ya ulinzi wa Polisi.
Kanusho hilo kutoka Makao Makuu ya Polisi limekuja kufuatia taarifa ya Polisi Mbagala iliyoandikwa kwenda kwa chama cha ACT Wazalendo kuzuia mkutano wa hadhara wa vijana wa chama hicho waliopanga kufanya leo Agosti 12,2024.
Naibu Katibu Mkuu Bara Benson Kigaila amewaeleza wanahabari kwamba viongozi hao wote wako chini ya mikono ya Polisi lakini Polisi hawataki kuwaonyesha wapi walipo hali inayowapa hofu juu ya usalama wao.
Chama cha ACT Wazalendo kimelaani na kukemea vikali vitisho vya Jeshi la Polisi na kukamatwa kwa viongozi wakuu wa CHADEMA na kuzuiwa kwa kongamano la vijana wa CHADEMA katika kuadhimisha siku ya vijana duniani iliyopangwa kufanyika leo Agosti 12, jijini Mbeya.
Jeshi la Polisi nchini Tanzania linawashikilia viongozi wakuu wa chama cha upinzani cha Chadema akiwemo Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe, aliyekuwa mgombea urais Tundu Lissu, na kuwakusanya mamia ya wafuasi wa vijana wa chama hicho
Shadrack Chaula anadaiwa kutekwa Agosti 2, 2024 ikiwa ni takribani siku 20 kupita tangu alipotoka Gereza la Ruanda lililoko mkoani Mbeya.
Taarifa iliyotolewa leo July 31,2024 na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano – TRC, Jamila Mbarouck imesema hitilafu I lisababisha umeme kukatika kituo cha kupoozea umeme namba 7 (Godegode) ambayo kitaalamu hujulikana kama (Instanteneous Overcurrent Protection Trip) majira ya saa 4:20 usiku
HRW ilisema iliwahoji karibu watu 100 kati ya Agosti 2022 na Desemba 2023, wakiwemo wanajamii ambao tayari walikuwa wamehamia kijiji cha Msomera huko Handeni na wengine wanaokabiliwa na uhamisho.