Ucheleweshaji wa tume huru wamtia wasiwasi Prof Lipumba
Chama cha Wananchi (CUF) nchini Tanzania, kimemuomba Rais wa nchi hiyo Samia Suluhu Hassan, atimize ahadi yake ya kujenga maridhiano na kuimarisha demokrasia ya vyama vingi, kwa kuhakikisha tume huru ya uchaguzi inapatikana kabla ya chaguzi zijazo.