Waziri wa zamani nchini Tanzania Geofrey Mwambe ashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za jinai
Taarifa ya polisi iliyotolewa leo, tarehe 12 Desemba 2025, imeeleza kuwa Mwambe ambaye aliwahi kuwa Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji na baadaye Wizara ya Viwanda na Biashara alikamatwa wakati wa operesheni ya kawaida ya kufuatilia masuala ya usalama jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, hatua za awali za kisheria kuhusu tuhuma zinazomkabili zinaendelea kukamilishwa.