Kikwete amjibu Polepole kuhusu utaratibu wa CCM: “Hakuna jambo jipya, utaratibu umeheshimiwa”
“Najua kulikuwepo na maneno au vijineno eti utaratibu umekiukwa na mimi nililaumiwa kwa jinsi nilivyosema pale kwenye mkutano mkuu, lakini nasema waliokuwa wanasema hayo ama hawafahamu utaratibu wa chama chetu na kama wanafahamu labda wamesahau au wanajifanya hamnazo,” alisema Kikwete.