Mkuu wa Fedha wa Uganda akabiliwa na mashtaka ya wizi wa dola Milioni 16
Afisa mkuu wa fedha wa Uganda, Lawrence Semakula, pamoja na wengine wanane, wamefunguliwa mashtaka ya udanganyifu na utakatishaji fedha kufuatia wizi wa karibu dola milioni 16 za Marekani zilizokuwa zimekusudiwa kulipia mikopo ya maendeleo, kulingana na nyaraka za mahakama.