Serikali ya Tanzania yataja vipaumbele mpango wa maendeleo 2024/25
Serikali imewasilisha mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa wa mwaka 2024/25. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo aliwasilisha mpango huo Dodoma jana katika kikao cha kamati ya bunge zima kilichoongozwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.