Siku 68 za Lissu gerezani, aeleza masaibu anayopitia
Licha ya kutohukumiwa, Lissu amedai amekuwa akishikiliwa kwenye eneo maalum la wafungwa wanaosubiri kunyongwa (death row) ndani ya Gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam.
Licha ya kutohukumiwa, Lissu amedai amekuwa akishikiliwa kwenye eneo maalum la wafungwa wanaosubiri kunyongwa (death row) ndani ya Gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, ameieleza Mahakama ya Kisutu kuwa ameamua kujiwakilisha mwenyewe katika shauri la uhaini yanayomkabili, akidai kunyimwa haki ya kuonana kwa faragha na mawakili wake tangu alipowekwa mahabusu zaidi ya miezi miwili iliyopita.
Jeshi la polisi nchini Kenya limetumia mabomu ya machozi leo Alhamisi kuwatawanya waandamanaji waliokuwa wakilaani mauaji ya mwalimu mmoja aliyefariki akiwa chini ya ulinzi wa polisi, hali iliyotishia kufunika juhudi za serikali kuwasilisha bajeti mpya bila kuchochea ghasia kama za mwaka uliopita.
Kwa mujibu wa CHADEMA, Msajili wa Vyama vya Siasa amekiuka Katiba kwa kudai kuwa uteuzi wa viongozi wa CHADEMA una dosari za kikatiba, akitaka nafasi hizo kujazwa upya huku akipuuzia mamlaka halali ya vikao vya chama vilivyoteua na kuthibitisha viongozi hao kwa mujibu wa Katiba ya chama.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limeendelea kulizingira Kanisa la Ufufuo na Uzima, linaloongozwa na Askofu Josephat Gwajima, huku baadhi ya waumini wa kanisa hilo wakishikiliwa kwa mahojiano, kufuatia agizo la Serikali la kulifunga kanisa hilo kwa madai ya ukiukaji wa sheria.
Katika video hiyo, Askofu Gwajima, ambaye pia ni kiongozi wa dini, alizungumza na wanahabari tarehe 24 Mei, 2025, akitoa maoni kuhusu mfululizo wa matukio ya utekaji yanayodaiwa kutokea nchini Tanzania. Maudhui hayo yalichapishwa kwenye chaneli ya The Chanzo Online TV kupitia YouTube.
Jeshi la Uganda (UPDF) limetangaza kusitisha mara moja ushirikiano wa kijeshi na Ujerumani, likimtuhumu Balozi wa Ujerumani nchini humo, Matthias Schauer, kwa kuendesha “shughuli za kihaini” ndani ya taifa hilo la Afrika Mashariki.
Amnesty International yafichua mateso makali wanayopitia wanawake wa Kenya wanaofanya kazi za ndani nchini Saudi Arabia, ikiwemo ubakaji, ubaguzi wa rangi, njaa, na utumwa wa kisasa unaofanyika chini ya mfumo wa Kafala.
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetangaza kuanzishwa kwa majimbo mapya nane ya uchaguzi pamoja na kubadilishwa kwa majina ya majimbo mengine 12, ikiwa ni maandalizi ya kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.
Mwanasiasa mkongwe Martha Karua ametangaza nia yake ya kugombea urais wa Kenya katika uchaguzi wa mwaka 2027, akisema kuwa nchi hiyo iko “katika hali ya vurugu kamili” kutokana na ufisadi, mauaji yanayotekelezwa na polisi, na kuzorota kwa uchumi.