Four in Tanzania gang rape video jailed for life
A Tanzanian court sentenced four men to life in prison Monday for a gang rape that shocked the country after a video of the assault went viral on social media
A Tanzanian court sentenced four men to life in prison Monday for a gang rape that shocked the country after a video of the assault went viral on social media
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu amesema anakusudia kuishtaki kampuni ya Tigo na Serikali ya Tanzania katika mahakama ya Uingereza kufuatia kampuni hiyo kushirikiana na Serikali katika kutoa taarifa zake na kumfatilia hadi kusababisha kushambuliwa kwake.
Inadaiwa kwamba Tigo ilitoa taarifa za simu na eneo la Lissu kwa mamlaka za Tanzania kwa muda wote wa saa katika wiki zilizotangulia kabla ya shambulio hilo lililotokea tarehe 7 Septemba 2017.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, ameeleza kuwa mwezi huu umejawa na maombolezo kwa chama hicho kutokana na yanayoendelea kutokea dhidi ya wanachama wake ambapo hadi sasa baadhi yao hawajulikani walipo tangu walipotekwa na wasiojulikana huku wengine wakiishia mikononi mwa polisi kwa kesi zinazotajwa kuwa ni za uchochezi.
Rais Samia Suluhu Hassan ametoa onyo kwa mabalozi waliotoa tamko kulaani mauaji ya kibao nchini, akisema kuwa Tanzania haitahitaji maelekezo kutoka kwa mtu yeyote kuhusu jinsi ya kuendesha mambo yake ya ndani.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Emmanuel Nchimbi, amekanusha vikali madai kwamba chama chake kinahusika na matukio ya utekaji na mauaji yanayoendelea nchini Tanzania. Nchimbi alisisitiza kuwa vitendo hivi vinachochewa na magenge ya uhalifu yenye lengo la kutafsiri CCM kama wauaji na kuchochea ugumu wa uhusiano kati ya chama hicho na wananchi.
Jeshi la Polisi Nchini Tanzania limetoa onyo kali na kupiga marufuku maandamano yaliyotangazwa na viongozi wa CHADEMA yatakayofanyika tarehe 23 Septemba 2024. Polisi wameonya kwamba mtu yeyote atakayepatikana akiingia barabarani atakabiliwa na hatua kali za kisheria.
Leo, Septemba 9,2024 mwili wa Ali Kibao, kada maarufu wa chama cha Chadema ambaye alifariki baada ya kutekwa umezikwa huku umati mkubwa wa watu umejitokeza kushuhudia safari yake ya mwisho iliyojaa huzuni ya kutafakarisha
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), Freeman Mbowe ametangaza kumfikisha Mahakamani aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Nyasa na Mbunge wa zamani wa chama hicho ambaye sasa ni kada wa CCM mchungaji Peter Msigwa kutokana na kauli za kumdhalilisha anazozitoa dhidi yake.
Kesi ya afande anayedaiwa kuwatuma vijana kubaka kwa kikundi na kumwingilia kinyume na maumbile binti mkazi wa Yombo Dovya jijini Dar es salaam, Fatma Kigondo inakuja leo baada ya mahakama kutoa hati ya wito kwa mara nyingine Agosti 23 mwaka huu.