42 wafariki kwa kunywa pombe yenye sumu nchini India

Mamia ya watu hufa kila mwaka nchini India kutokana na pombe ya bei nafuu inayotengenezwa kwenye viwanda vya kutengeneza pombe.

0

Takriban watu 42 wamefariki na wengine karibu 100 wamelazwa hospitalini magharibi mwa India baada ya kunywa pombe yenye sumu.

Kufuatia tukio hilo mamlaka imeamuru msako mkali kufanyika dhidi ya wafanyabiashara wa pombe.

Makumi ya watu waliugua mapema wiki hii baada ya kunywa methanol aina ya pombe yenye sumu ambayo wakati mwingine hutumika kama dawa ya kuzuia baridi ambayo huuzwa katika vijiji kadhaa katika jimbo la Gujarat.

“Uchunguzi umebaini kuwa waathiriwa walikuwa wametumia methanol ya kiwango cha viwandani ambayo ilisababisha vifo,” Waziri wa Mambo ya Ndani wa Jimbo Harsh Sanghavi alisema katika taarifa.

Sanghavi alisema kuwa watu 97 wamelazwa hospitalini kwa matibabu, huku wawili wakiwa katika hali mbaya.

Gujarat, jimbo la nyumbani kwa Waziri Mkuu Narendra Modi, ni moja ya majimbo kadhaa nchini India ambapo unywaji na uuzaji wa vileo ni kinyume cha sheria.

Mamlaka imevamia maduka ya pombe haramu kote Gujarat na kuwakamata watu kadhaa.

Mamia ya watu hufa kila mwaka nchini India kutokana na pombe ya bei nafuu inayotengenezwa kwenye viwanda vya kutengeneza pombe.

Kati ya wastani wa lita bilioni tano za pombe zinazolewa kila mwaka nchini, karibu asilimia 40 huzalishwa kinyume cha sheria, kulingana na Shirika la Mvinyo la India.

Pombe mara nyingi hutiwa methanoli ili kuongeza nguvu yake. Ikimezwa, methanoli inaweza kusababisha upofu, uharibifu wa ini na kifo.

Mwaka jana, watu 98 walikufa katika jimbo la kaskazini la Punjab baada ya kunywa pombe ya boti.

Na mnamo 2019, zaidi ya watu 150 walifariki katika tukio kama hilo kaskazini mashariki mwa jimbo la Assam, wengi wao wakiwa wafanyikazi wa mashamba ya chai.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted