Biashara ya ngono yaongezeka kwa wakimbizi wa ndani DRC
Taarifa iliyotolewa jana na shirika hilo kutoka Geneva Uswisi imesema ukosefu wa amani huko mashariki mwa DRC umesababisha watu kuwa na hali mbaya ya kimaisha na ukiukaji wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na unyanyasaji wa kijinsia, unaowakabiliwa zaidi ya wakimbizi wa ndani milioni 6.2.