Bunge la Ulaya laitaka Tume ya Ulaya kusitisha msaada wa euro milioni 156 kwa Tanzania
Wabunge wa Bunge la Ulaya wamepitisha azimio linaloitaka Tume ya Ulaya kuondoa pendekezo lake la kutoa msaada wa euro milioni 156 kwa Tanzania katika mwaka 2026, wakieleza kuwa hali ya haki za binadamu, demokrasia na utawala wa sheria nchini bado inatia wasiwasi.