ICJ kusikiliza kesi ya Kihistoria ya mauaji ya kimbarı ya Afrika Kusini dhidi ya Israel

Kesi ya mauaji ya halaiki iliyowasilishwa na Afrika Kusini dhidi ya Israel katika Ukanda wa Gaza inasikilizwa, leo Alhamisi, Januari 11, na pia Ijumaa, mbele ya Mahakama ya...

0

Kesi ya mauaji ya halaiki iliyowasilishwa na Afrika Kusini dhidi ya Israel katika Ukanda wa Gaza inasikilizwa, leo Alhamisi, Januari 11, na pia Ijumaa, mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki huko Hague (ICJ), nchini Uholanzi. Afrika Kusini iliwasilisha malalamiko yake mbele ya taasisi hii ya Haki ya Umoja wa Mataifa mwezi uliopita kuiomba kutoa uamuzi juu ya uwezekano wa vitendo vya “mauaji ya kimbari” katika Ukanda wa Gaza. Ni utaratibu wa hatua nyingi ambao unafunguliwa Alhamisi hii.

Afrika Kusini inaishutumu Israel, katika waraka wa kurasa 84, kwa kukiuka Mkataba wa Kuzuia na Kuadhibu Uhalifu wa Mauaji ya Kimbari, na inaomba mahakama hii ya Umoja wa Mataifa yenye makao yake makuu mjini Hague, ambayo inadhibiti mizozo kati ya Mataifa, kuchukua hatua za dharura. Pretoria ina nafasi Alhamisi hii, na Ijumaa, itakuwa zamu ya Israeli kujibu tuhuma dhidi yake.

Kama ukumbusho, sambamba na utaratibu huu katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ofisi ya mwendesha mashitaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) ilianza kuchunguza kwa upande wake mashambulizi ya Hamas yaliyofanywa Oktoba 7, na pia vita ambayo inaendelea kuukumba Ukanda wa Gaza tangu wakati huo. Lakini ICC inaweza tu kuhukumu watu binafsi na si mataifa.

Afrika Kusini itaeleza kwa nini inazingatia hatua za Israel kujumuisha vitendo vya “mauaji ya halaiki”.

Nchi hizo mbili kila moja zimeweza kuteua jaji ambaye atashirikia na mahakimu wengine. Kwa upande wa Israel, ni Aharon Barak, rais wa zamani wa Mahakama ya Juu ya nchi yake, aliyenusurika na Shoah. Na Pretoria imemteua Dikgang Moseneke, ambaye pia alihudumu katika Mahakama ya Katiba ya nchi yake, na ambaye ni mfungwa wa zamani wa Kisiwa cha Robben.

“Nchi zina wajibu wa kuzuia mauaji ya kimbari”

Israel tayari imekataa “kwa kuchukizwa” kile kinachoelezewa huko Jerusalem na Tel Aviv kama “kuchafuliwa” na Afrika Kusini. Kwa sababu machoni pa Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu, jeshi la nchi yake linajiendesha “kwa maadili yasiyo na kifani.” Ikiwa ICJ itachukua hatua hizi, hakuna chochote cha kusema kwamba Israeli itatii.

Mipaka ya haki ya kimataifa inajulikana. Kwa mfano, Mahakama ya Kimataifa ya Haki, iliamuru Urusi kukomesha mashambulizi yake nchini Ukraine, bila mafanikio. Lakini François Dubuisson, mtaalamu wa sheria za kimataifa katika Chuo Kikuu Huria cha Brussels, anasema hii inaweza kuongeza shinikizo la kimataifa.

“Chini ya Mkataba wa Mauaji ya Kimbari, Nchi Wanachama zote zina wajibu wa kuzuia mauaji ya kimbari,” François Dubuisson anakumbusha, akizungumza na Nicolas Falez, wa kitengo cha kimataifa cha RFI.

Ikiwa Mahakama itasema kwamba ili kuzuia mauaji ya halaiki, mlolongo mzima wa hatua lazima uchukuliwe, ambayo itahimiza Mataifa yote kutoa shinikizo kubwa zaidi.

Kwa hivyo, Israeli inaweza kujipata, anahitimisha mwanasheria, chini ya shinikizo “ili ichukue safu ya hatua: ama kusitisha mashambulizi ya anga, au angalau kuitisha mapigano kwa muda”. François Dubuisson anaona katika utaratibu huu katika ICJ kazi kubwa ya Afrika Kusini inayoibwa israeli.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted