Rwanda yadhimisha miaka 30 ya mauaji ya kimbari

Rais wa Rwanda Paul Kagame, ameipongeza Kenya kwa wajibu wake mkubwa katika kujengwa upya kwa taifa la Rwanda baada ya mauaji ya kimbari yaliyotekelezwa mwaka 1994.

0

Rais wa Rwanda Paul Kagame, ameipongeza Kenya kwa wajibu wake mkubwa katika kujengwa upya kwa taifa la Rwanda baada ya mauaji ya kimbari yaliyotekelezwa mwaka 1994.

Rais Kagame alisema Kenya iliwahifadhi wakimbizi wengi waliokuwa wakitoroka Rwanda wakati wa kipindi hicho kigumu.

People hold candles during a night vigil at the Kigali Arena on the 30th Anniversary of the 1994 Rwandan genocide in Kigali on April 7, 2024. – Rwanda on Sunday paid solemn tribute to genocide victims, 30 years after a vicious campaign orchestrated by Hutu extremists tore apart the country, as neighbours turned on each other in one of the bloodiest massacres of the 20th century. The killing spree, which lasted 100 days before the Rwandan Patriotic Front (RPF) rebel militia took Kigali in July 1994, claimed the lives of around 800,000 people, largely Tutsis but also moderate Hutus. (Photo by Guillem Sartorio / AFP)

Rais Kagame aliwaambia marais na viongozi wa serikali, mabalozi na wakuu wa jumbe mbalimbali jijini Kigali kuwa Kenya ilikuwa miongoni mwa mataifa yaliyosaidia kujengwa na kufufuliwa upya kwa taifa la sasa la Rwanda.

Alikuwa akiongea katika eneo la BK Arena jijini Kigali Rwanda wakati wa maadhimisho ya 30 ya kitaifa tangu kutokea kwa mauaji ya kimbari  ya Rwanda yaliyosababisha vifo vya mamilioni ya watu mwaka wa 1994.

Kenya, pamoja na mataifa mengine, ilihifadhi idadi kubwa ya wakimbizi wa Rwanda na kuwapatia makao,” alisema Rais huyo wa Rwanda.

Kenya iliwakilishwa na naibu wa rais Rigathi Gachagua ambaye alimwakilisha rais William Ruto.

Gachagua aliweka shada la maua katika eneo la ukumbusho la Kigali Genocide Memorial, kwa heshima ya waathiriwa wa mauaji hayo ya halaiki ya mwaka wa 1994.

Kituo hicho cha ukumbusho ndipo walipozikwa mamilioni ya watu waliouawa katika kipindi cha miezi mitatu cha mauaji hayo ya halaiki.

Siku ya jumapili iliadhimisha mwanzo wa maadhimisho ya siku mia moja ya kumbukumbu hizo.

Baadhi ya viongozi wa dunia waliohudhuria sherehe hiyo ni pamoja na aliyekuwa Rais wa Marekani Bill Clinton, Rais wa Sudan Kusini Cyril Ramaphosa, Rais wa Sudan Kusini Salva Kirr, Rais wa Samia Sulubu na Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed miongoni mwa wengine.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted