Kesi Ya Uhaini Ya Lissu- Shahidi: Kutoa Maudhui ya Uchochezi ni Uhaini
Lissu: Waeleze majaji kwamba mtu anaetoa maudhui ya Uchochezi ni kosa la Uhaini. Je maudhui yenye Uchochezi kwa umma ni kosa la Uhaini au sio
Shahidi :Ni kosa la Uhaini
Lissu: Waeleze majaji kwamba mtu anaetoa maudhui ya Uchochezi ni kosa la Uhaini. Je maudhui yenye Uchochezi kwa umma ni kosa la Uhaini au sio
Shahidi :Ni kosa la Uhaini
Shahidi huyo ambaye ni Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) George Wilbart Bagemu, mwenye umri wa miaka 48, ambaye ni afisa mwandamizi wa Jeshi la Polisi mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka ishirini katika taaluma ya upelelezi.
Akijibu ripoti iliyotolewa na Shirika la Kutetea Haki za Binadamu, Human Rights Watch (HRW), Msemaji wa Serikali, Gerson Msigwa, amesema madai hayo hayana msingi na yanapotosha hali halisi ya nchi.
Goodall, aliyebobea katika utafiti wa sokwe pori na baadaye kuwa mwanaharakati wa mazingira, alibadilisha mapenzi yake ya wanyamapori kuwa kampeni ya maisha yote. Safari yake ilimtoa kutoka kijiji cha pwani kusini mwa Uingereza hadi Afrika, na hatimaye kumzungusha duniani kote akijitahidi kuelewa sokwe na nafasi ya binadamu katika kulinda makazi yao pamoja na afya ya sayari kwa ujumla.
Kisiwa hicho cha Bahari ya Hindi kilikuwa kinangoja uteuzi wa waziri mkuu mpya baada ya Rais Andry Rajoelina kuvunja baraza lake lote la mawaziri Jumatatu, hatua aliyochukua kutuliza maandamano yaliyoshika kasi tangu Septemba 25 kutokana na malalamiko ya uongozi mbaya pamoja na ukosefu wa maji na umeme.
Wanaharakati wa mitandaoni, Innocent Paul Chuwa maarufu kama Kiduku, na Farida Mikoroti, waliokamatwa kwa tuhuma za makosa ya mtandao, wameachiwa kwa dhamana kutoka Kituo Kikuu cha Polisi cha Kati (Central Police) Dar es Salaam, Jumatano Oktoba 01, 2025.
Kwa mujibu wa taarifa, mtuhumiwa ambaye ni mama mdogo wa mama mzazi wa marehemu, anadaiwa kumpiga mtoto huyo maeneo mbalimbali ya mwili wake kisha kumkaba shingo na kusababisha kifo chake.
Waandamanaji nchini Madagascar wameitisha maandamano mapya leo Jumanne, siku moja baada ya Rais wa nchi hiyo Andry Rajoelina kuvunja serikali yake kwa lengo la kutuliza ghasia zilizosababisha vifo vya watu 22, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.
Wiki iliyopita maandamano ya siku mbili yaliibuka na kusababisha makabiliano kati ya vijana na polisi. Waandamanaji, waliyoitishwa kupitia mitandao ya kijamii na vuguvugu la “Gen Z”, walilalamikia kukatika kwa maji na umeme kunakolikithiri katika taifa hilo maskini.
Mwanasiasa huyo mkongwe, ambaye aliwahi kushika madaraka kuanzia mwaka 2014 hadi 2020, amechaguliwa tena kwa kura karibu asilimia 57 ili kuongoza taifa hilo lenye watu milioni 21 wengi wao wakiwa maskini.