Kesi Ya Tundu Lissu Yaahirishwa Hadi Aprili 28
Wakili Alute Mghwai ambaye pia ni ndugu wa Lissu, alieleza kuwa hali anayoishi Lissu akiwa gerezani ni kama tayari ameshahukumiwa, jambo linalokiuka Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Wakili Alute Mghwai ambaye pia ni ndugu wa Lissu, alieleza kuwa hali anayoishi Lissu akiwa gerezani ni kama tayari ameshahukumiwa, jambo linalokiuka Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza limetoa tahadhari kwa wananchi na wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wanaopanga kufanya mikusanyiko na maandamano ya kuishinikiza Serikali kuachiwa huru Mwenyekiti wa chama hicho Taifa ambaye kesho Aprili 24,2025 atafikishwa mahakamani.
Thiam, ambaye hivi karibuni aliteuliwa kuwa kiongozi wa chama cha Democratic Party of Ivory Coast (PDCI), ameondolewa kwa madai kuwa alipoteza uraia wa Ivory Coast baada ya kupata uraia wa Ufaransa mwaka 1987.
Mahakama Kuu ya Marekani, ambayo ina wingi wa majaji wa mrengo wa kihafidhina, inatarajiwa kusikiliza kesi leo Jumanne kuhusu iwapo wazazi wana haki ya kidini kuwazuia watoto wao kuhudhuria madarasa yanayosoma au kujadili vitabu vyenye maudhui ya LGBTQ.
Francis, ambaye alijulikana kwa jitihada zake za kufanya mageuzi ndani ya Kanisa Katoliki na aliwahamasisha wengi, alifariki akiwa na umri wa miaka 88.
Ametoa agizo hilo leo Jumatano (Aprili 16, 2025) alipokagua maendeleo ya ukarabati wa madaraja katika maeneo ya Matandu na Somanga Mtama, Wilaya Kilwa Mkoani Lindi kwenye barabara kuu ya Dar es Salaam – Lindi yaliyokuwa yamekatika kufuatia mvua zinazonyesha nchini.
Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu, Amnesty International, limeitaka serikali ya Tanzania kumwachilia mara moja na bila masharti yoyote kiongozi wa chama cha upinzani Chadema, Tundu Lissu, aliyekamatwa na kufunguliwa mashtaka ya uhaini.
Chama cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi wake kuhusu kutoweka kwa matumaini ya mageuzi katika sheria za uchaguzi, kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Lissu alikamatwa Aprili 9, 2025, wilayani Mbinga mkoani Ruvuma muda mfupi baada ya kuhutubia mkutano wa hadhara. Usiku huo huo alisafirishwa kwa magari hadi Dar es Salaam na kufikishwa katika Kituo Kikuu cha Polisi (Central), kabla ya kupelekwa mahakamani leo asubuhi.
Haya yameelezwa leo Aprili 9,2025, bungeni jijini Dodoma na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2025/2026, ambapo ameeleza kuwa takwimu zilizopo watu 1,690,948 wanaishi na virusi vya UKIMWI (WAVIU).