Amnesty International yaitaka Tanzania kumwachilia huru kiongozi wa upinzani Tundu Lissu
Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu, Amnesty International, limeitaka serikali ya Tanzania kumwachilia mara moja na bila masharti yoyote kiongozi wa chama cha upinzani Chadema, Tundu Lissu, aliyekamatwa na kufunguliwa mashtaka ya uhaini.