Kesi la Lissu: Jamhuri kutafakari uamuzi wa Mahakama kuhusu mapingamizi ya Lissu
Upande wa Jamhuri ukiwakilishwa na Wakili Mkuu wa Serikali Renatus Mkude ulisema baada ya kumaliza ushahidi wa shahidi huyo, unakwenda kutafakari maamuzi yaliyotolewa na Mahakama Kuu juu ya mapingamizi mawili ambayo yaliletwa na mshtakiwa kuhusiana na vielelezo ambavyo Mahakama imevikataa.