Lissu:Mifumo ya viwango vya kodi inapaswa kuwa wazi.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tanzania Bara, Tundu Lissu amesema mifumo na viwango vya kodi inapaswa kuwa wazi ili anayelipa ajue analipa kiasi gani na anayekusanya ajue anakusanya kiasi gani.