John Mnyika Aanza Kutoa Ushahidi Wa Utetezi Katika Kesi Ya Lissu
Sehemu kubwa ya ushahidi wa Mnyika imejikita katika mkutano wa CHADEMA uliofanyika Aprili 3, 2025 katika makao makuu ya chama Mikocheni, Dar es Salaam. Mnyika ameieleza Mahakama kuwa mkutano huo ulikuwa wa ndani wa chama, uliwahusisha watia nia wa uchaguzi wa mwaka 2025 pamoja na viongozi na waandishi wa habari.