Aliyekuwa Naibu Waziri wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, atuhumiwa kumfanyia ukatili mfanyakazi wake
Gekul ambaye ni Mbunge wa Chama cha Mapinduzi CCM, anatuhumiwa kutoa maelekezo kwa kundi la vijana wake kumwingizia chupa sehemu ya haja kubwa mfanyakazi wake, Hashim Ally au kumpiga risasi kwa madai kwamba alitumwa kimkakati kwenda kwenye hoteli yake ya Paleii Lake View Garden.