CHADEMA yasusia uchaguzi mdogo madiwani, yaitaka Serikali kuheshimu uamuzi wa Mahakama ya Afrika
Katika taarifa iliyotolewa na CHADEMA imeeleza sababu za kutoshiriki uchaguzi huo ambapo imesema uchaguzi huo utasimimamiwa na Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya jambo ambalo ni kinyume na uamuzi wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu uliotolewa Juni 13, baina ya Chacha Wangwe dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.