Mbunge wa Ngorongoro ashangazwa Polisi kumkamata bila kibali cha Spika
Mbunge wa Ngorongoro Emmanuel Ole Shangai (CCM),ameshangazwa na hatua ya polisi kumkamata bila kibali cha Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, kama ambavyo taratibu za ukamatwaji zinapaswa kufanywa kwa wabunge kutokana na kinga ya bunge waliyonayo.