Mtafiti wa Colombia auawa na tembo nchini Uganda

Mtafiti kutoka Colombia amekanyagwa hadi kufa na tembo katika Mbuga ya Kitaifa ya Kibale

0

Mtafiti kutoka Colombia amekanyagwa hadi kufa na tembo katika Mbuga ya Kitaifa ya Kibale magharibi mwa Uganda, mamlaka ya hifadhi za taifa nchini humo ilisema Jumatatu.

Sebastian Ramirez Amaya, kutoka Chuo Kikuu cha Arizona State nchini Marekani, alikuwa na mtafiti mwingine na mwongozaji katika mbuga hiyo ya taifa, inayojulikana kwa kituo chake cha wanyamapori na utafiti, alipofariki siku ya Jumapili.

“Walikutana na tembo kighafla, na kuwalazimisha kukimbia pande tofauti,” mamlaka ya mbuga za kitaifa ya Uganda ilisema katika taarifa siku ya Jumatatu.

“Tembo huyo alimfukuza Sebastian na kumkanyaga, na kusababisha kifo chake,” taarifa hiyo iliongeza, ikisema kwamba hilo ni tukio la kwanza la mauaji katika mbuga hiyo kwa miaka 50.

Mnamo Januari, mtalii mmoja wa Saudia alikanyagwa hadi kufa na tembo alipokuwa akizuru mbuga nyingine maarufu nchini Uganda, Murchison Falls, baada ya kuacha gari alilokuwa akisafiria na kuzunguka mbugani kwa mguu.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted