Maelfu ya watu wanawakimbia waasi wa Kiislamu nchini DR Congo

Wanatoroka mfululizo wa mashambulizi ya waasi wa Kiislamu wa Allied Democratic Forces (ADF) katika jimbo hilo.

0

Wafanyakazi wa kutoa misaada katika jimbo la Ituri mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wanasema maelfu ya watu waliotoroka makazi yao wamekuwa wakiwasili katika mji mkuu wa eneo hilo, Beni.

Wanatoroka mfululizo wa mashambulizi ya waasi wa Kiislamu wa Allied Democratic Forces (ADF) katika jimbo hilo.

Zaidi ya watu 90 wameuawa katika muda wa wiki moja iliyopita katika mashambulizi dhidi ya vijiji 18.

Majaribio ya majeshi ya DR Congo na Uganda kuwaangamiza waasi yamepiga hatua kidogo.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted