Mapinduzi ya Niger: ECOWAS yaungwa mkono na mataifa ya Afrika ya Kati

Rais Tinubu alikiri wajumbe kadhaa wa kidiplomasia ambao wameingilia kati katika kutatua mgogoro wa Niger akisisitiza kwamba "Kuingilia utawala wa kidemokrasia hakukubaliki kwa ECOWAS."

0

Jumuiya ya kanda ya Afrika ya Kati ECCAS, imetoa uungaji mkono wake kwa juhudi za wenzao wa Afrika Magharibi, ECOWAS katika kupindua mapinduzi ya Niger na kurejesha utaratibu wa kikatiba, Rais wa Nigeria na Mwenyekiti wa ECOWAS Bola Tinubu alisema katika taarifa, Jumanne baada ya ziara ya mjumbe maalumu wa Rais wa Gabon na Mwenyekiti wa ECCAS, Ali Bongo Ondimba kwenye ikulu ya Abuja, mji mkuu wa Nigeria.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Gabon, Hermann Immongault, alisema Rais Bongo “alilaani vikali” mapinduzi ya Niger na kuunga mkono hatua zote za ECOWAS zilizochukuliwa kurejesha demokrasia nchini Niger.

Rais Tinubu alikiri wajumbe kadhaa wa kidiplomasia ambao wameingilia kati katika kutatua mgogoro wa Niger akisisitiza kwamba “Kuingilia utawala wa kidemokrasia hakukubaliki kwa ECOWAS.”

“Ninaelewa hofu ya watu wetu kwa aina yoyote ya hatua za kijeshi. Tunajitahidi kuweka vikwazo hivyo, na tunavifuata kikamilifu.” Rais Tinubu aliongeza.

ECOWAS ilikuwa imetoa vikwazo kadhaa ikiwa ni pamoja na kufungwa kwa mpaka nchini Niger ambapo mapinduzi ya kijeshi yalimwondoa madarakani Rais Mohamed Bazoum mnamo Julai 26.

Jumuiya ya kikanda ilisema itapeleka kikosi cha ECOWAS nchini Niger ili kurejesha utulivu wa kikatiba kufuatia kumalizika kwa makataa ambayo ilitolewa kwa viongozi wa mapinduzi kumrejesha madarakani Rais aliyeng’olewa madarakani.

Hata hivyo haikutoa muda wa matumizi ya nguvu ambayo ilisema ni “chaguo la mwisho” iwapo chaguzi zote za kidiplomasia na kisiasa zitashindwa.

Wakuu wa ulinzi kutoka eneo hilo wanakutana mjini Accra siku ya Alhamisi na Ijumaa ili kujadili uwezekano wa suluhu la mgogoro wa Niger.

Mapinduzi ya kijeshi yamevutia hisia za kimataifa huku serikali nyingi za kigeni zikitoa wito wa kutatuliwa kwa amani mgogoro huo.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Antony Blinken Jumanne alisema Marekani inaamini bado kuna “nafasi ya diplomasia” katika kufanikisha kurejeshwa kwa utaratibu wa kikatiba.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted