Mahakama Kuu yaidhinisha kiapo cha ziada kesi ya kutekwa kwa Polepole
Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam imeridhia maombi ya mawakili wa aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, kuwasilisha kiapo cha ziada katika shauri la maombi ya kutekwa kwa utaratibu wa kisheria (Habeas Corpus).